CARNELLO ALVAREZ AMTWANGA AMIR KHAN KWA KO.

images
Carmello Alvarez amedhihirisha kwamba yeye ni mwamba kwa kumtwanga na KO mpinzani wake Amir Khan katika raundi ya sita katika pambano lililovutia watu wengi mjini Las Vegas Nv.Wachambuzi walijiuliza je uzoefu ni dawa lakini haikuwezekana maana Amir Khan alitamba katika raundi za mwanzo lakini baadae mambo yakawa magumu.
Khan hakuweza kuvumilia na kukjwepa makonde maziyto ya Carnello Alvarez na kutokana na hilo basi nafikri wakati wa kujizulu kwa Khan sasa ni dhahiri umewadia.
Khan ambaye pamoja na kushindwa ametia kibindoni dola milioni 2 nalijitapa kabla ya pambano hilo kwamba staili yake imebadilika na ataweza kupata ushindi lakini aligonga mwamba.

Mnakaribishwa ibada ya misa ya kiswahili.

Misa

Mnakaribishwa sana
kwenye ibada ya misa takatifu kwa lugha ya kiswahili. Ibada hii inapoadhimishwa kwa siku ya Kina-Mama wote.

Ibada itafanyika katika kanisa takatifu katoliki la
Mtakatifu Edward (St Edward Parish)

901 Poplar Grove St,
Baltimore, MD 21216,
Phone: (410) 362-2000

Jumapili Tarehe 8 May 2016,
Saa nane kamili mchana (2:00 PM).

Karibu sana na unaombwa uwataarifu na kuwakaribisha
ndugu, marafiki na jamaa zako.

Karibu pia kujiunga kwa mawasiliano
ya barua pepe anwani.
WauminiWakatoliki@gmail.com

Kwa niaba ya Fr. Honest Munish ni katibu Tibruss Minja.

Misa ya msiba wa uncle George Sebo

IMG_8682Baadhia ya wakes wa DMV na vitongoji vyake wakifuatilia ibada ya mazishi ya George Sebo aliyekuwa pia mwenyekiti wa CCM DMV na pia kipenzi cha wengi mwishoni mwa juma katikla kanisa la Evangel Cathedral Upper Marlboro Md.

WATANZANIA WENGI WANAKOSA FURSA ZA KIMAENDELEO KUTOKANA NA KUTOJUA LUGHA

Charles Mombeki (Kulia) ambae ni Mkurugenzi wa International Language Training Centre akizungumza na George Binagi kuhusiana na Umhimu wa Watanzania kujifunza lugha za Kimataifa hususani Kiingereza kwa ajili ya kuendana na muingiliano wa Kimataifa uliopo katika shughuli mbalimbali ikiwemo biashara.
“Watanzania wengi wanakosa fursa mbalimbali zilizopo. Wengine wanakosa fursa za kibiashara pamoja na kazi kutoka katika Mashirika na Makampuni mbalimbali duniani kutokana na kushindwa kufahamu lugha za Kimataifa hususani kiingereza, Kijerumani, Kifarasa, Kichina na hata lugha nyingine. Hivyo niwasihi waamue kujifunza lugha, kwa kuwa lugha inafungua milango ya mafanikio maishani”. Anasema Mombeki.
Anasema, Watanzania wawaandae watoto wao katika lugha ya Kiingereza katika kupata elimu, akiunga mkono shule za watu ama Mashirika binafsi kutumia lugha ya Kiingereza kufundishia, tofauti na ilivyo kwa shule za Serikali kutumia lugha ya Kiswahili katika kufundishia katika shule za msingi akitanabaisha kwamba bado kiswahili hakijawa na nafasi kubwa kutumika kimataifa kama ilivyo kiingereza ambayo ni lugha inayowaunganisha watu wote Kimataifa. 
Mombeki anadokeza kuwa wanafunzi waliofundishwa kwa misingi ya kiingereza tangu wakiwa wadogo wana nafasi kubwa ya kufikia malengo yao ikilinganishwa na wale walioanza elimu yao ya  awali na msingi kwa lugha ya kiswahili.
Anabainisha kuwa kuna wanafunzi wengi kutoka Mataifa ya Afrika, Amerika na Ulaya wanapenda kufika katika Centre hiyo ambayo ilianza kutoa elimu ya lugha mbalimbali tangu mwaka 1998. Pia inafundisha lugha ya Kiswahili pamoja na lugha za asili ikiwemo Kisukuma pamoja na Mila na Desturi za Tanzania.
Imeandaliwa na George Binagi

TANZIA DMV NA TANZANIA LETICIA NYERERE HATUNAE TENA.

a37aac512fe42933bc5b4a8a74b053adAliyekua Mbunge viti maalum Leticia Nyerere ameaga Dunia Jumapili katika Hospitali ya Doctors Community iliyopo Lan ham, Maryland. Msiba DMV upo 9004 Brightlea Court, Lanham, MD 20706. Taarifa zaidi zitakujia baadae R.I.P. mama yetu mpendwa tulikupenda lakini Mwenyezi Mungu amekupenda zaidi.

SERIKALI YATOA TAARIFA YA MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI TZ

<a href=”http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/IMG_0652.jpg” rel=”attachment wp-att-154740″><img class=”aligncenter size-full wp-image-154740″ src=”http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/IMG_0652.jpg” alt=”IMG_0652″ width=”640″ height=”427″ /></a>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000080;”><em><strong>Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangalla akitoa tamko kwa umma, kuhusu mwenendo wa ugonjwa wa kipindupindu katika mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) ofisini kwake jijini Dar es Salaam. Pichani chini kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Afya (Kaimu Mkurugenzi), Michael John.</strong></em></span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangalla ametoa tamko kwa umma, kuhusu mwenendo wa ugonjwa wa kipindupindu ulioanza tarehe 15 Agosti, 2015 katika mkoa wa Dar es Salaam na kusambaa kwa kasi katika Mikoa mingine 21 ya Tanzania Bara ambayo  ni  Pwani, Morogoro, Iringa, Kilimanjaro, Dodoma, Kigoma, Geita, Mara, Manyara, Arusha, Shinyanga, Tabora, Singida, Tanga, Lindi, Rukwa, Kagera, Katavi, Mbeya na Mwanza na Simiyu.</span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Tangu ugonjwa huu uanze, jumla ya watu 12,810 wameugua Kipindupindu, na kati yao jumla ya watu 202 wameshafariki kwa ugonjwa huu ambayo ni sawa na asilimia 1.6 ya waliougua. Katika kipindi cha wiki iliyoanza tarehe 28 Desemba 2015 hadi tarehe 3 Januari 2016, kumekuwa na jumla ya wagonjwa walioripotiwa 590 na vifo 6, ambayo ni asilimia 0.01 ya wagonjwa wote. Mkoa wa Mara (Musoma Mjini) ndio ulikuwa unaongoza kwa kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu ukifuatiwa na Singida (Iramba), Morogoro (Morogoro Vijijini) na Manyara (Simanjiro).</span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Takwimu zinaonyesha kuwa licha ya kuwa na nafuu katika wiki ya nyuma, wiki hii kasi ya maambukizi inaonesha kupanda tena kwenye mikoa ya Mwanza na Arusha.  Katika mkoa wa Arusha, maambukizi yamepanda kutoka wagonjwa wapya 60 hadi 111 kwa wiki.  Katika mkoa wa Mwanza, kasi ya maambukizi imepanda kutoka wagonjwa wapya 45 hadi 66 kwa wiki.</span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Kasi ya maambukizi ya Kipindupindu katika wiki iliyopita imepungua kwa kiasi kikubwa katika mikoa ya Mbeya na Tanga. Aidha, mikoa ya Dar-es-Salaam na Lindi haijaripoti mgonjwa yeyote mpya wa Kipindupindu katika wiki iliyopita. Tunawapongeza kwa hatua hii kutokana na juhudi zinazofanywa na wadau ambao kwa pamoja, wameshirikiana kudhibiti ugonjwa huu kwa karibu zaidi.</span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kwa kushirikiana na Sekta nyingine husika, wadau wa maendeleo na wadau wengine inaendelea kukabiliana na ugonjwa huu kwa njia mbalimbali. Kikosi kazi maalum chini ya uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu kinakamilisha mpango unaoshirikisha Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto , TAMISEMI, Wizara ya Maji na Umwagiliaji, DAWASCO, DAWASA, Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi pamoja  na Sekretariat ya Mkoa wa Dar-es-Salaam, kwa ajili ya kuhakikisha kuwa mikakati ya kupambana na ugonjwa huu inakuwa jumuishi na ya haraka.</span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Bado Wizara inaendelea kusisitiza kuwa, ili kudhibiti ugonjwa na kuokoa vifo vinavyotokana na ugonjwa huu, wananchi wanasisitizwa kunywa maji yaliyo safi na salama, kuepuka kula chakula kilichoandaliwa katika mazingira yasiyo safi na salama, kunawa mikono kwa sabuni na maji safi  yanayotiririka:-                kabla na baada ya kula, baada ya kutoka chooni,Baada ya kumnawisha mtoto aliyejisaidia na baada ya kumhudumia mgonjwa</span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Aidha, ni muhimu kuhakikisha kuwa wananchi wanatumia vyoo wakati wote na kutokujisaidia ovyo katika vyanzo vya maji vya mito, mabwawa na ziwani. Wizara ilishapiga marufuku kuuza matunda yaliyokatwa na vyakula barabarani katika mazingira yasiyo safi na salama.  Hivyo, Mamlaka za Mikoa na Halmashauri pamoja na watendaji ambao ni  Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya, Maafisa Afya, ziendelee kutoa taarifa kuhusu utekelezaji wa jambo hili.</span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Wizara inapeleka tena timu za wataalm katika mikoa iliyoathirika zaidi na kipindupindu ambayo ni Simiyu, Mara, Morogoro, Manyara, Singida, Arusha na Mwanza.  Timu hizi zitaungana na timu za mkoa wa wilaya kusaidia kudhibiti ugonjwa huu.</span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Hitimisho</span></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000000;”>Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inaendelea kukumbusha kuwa, mikoa ambayo bado haijaathirika ichukue hatua za tahadhari za kuzuia ili isipate mgonjwa yeyote wa Kipindupindu.</span></p>
<p style=”text-align: center;”><a href=”http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/IMG_0622.jpg” rel=”attachment wp-att-154739″><img class=”aligncenter size-full wp-image-154739″ src=”http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/IMG_0622.jpg” alt=”IMG_0622″ width=”640″ height=”460″ /></a></p>
<p style=”text-align: center;”><a href=”http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/IMG_0675.jpg” rel=”attachment wp-att-154741″><img class=”aligncenter size-full wp-image-154741″ src=”http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/IMG_0675.jpg” alt=”IMG_0675″ width=”640″ height=”427″ /></a></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000080;”><em><strong>Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) hapa nchini, Dk Rufaro Chatora (kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano makao makuu ya wizara hiyo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangalla.</strong></em></span></p>
<p style=”text-align: center;”><a href=”http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/IMG_0625.jpg” rel=”attachment wp-att-154742″><img class=”aligncenter size-full wp-image-154742″ src=”http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/IMG_0625.jpg” alt=”IMG_0625″ width=”640″ height=”427″ /></a></p>
<p style=”text-align: center;”><span style=”color: #000080;”><em><strong>Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Afya (walioketi) na waandishi wa habari katika mkutano huo.</strong></em></span><a href=”http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/IMG_0625.jpg” rel=”attachment wp-att-154742″>
</a></p>