Taswira ya choo cha kisasa kilichojengwa kwenye machinjio hiyo.
Archives
JK AMUWAKILISHA RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI MAZISHI YA LUCY KIBAKI NCHINI KENYA
RAIS DKT MAGUFULI ASHIRIKI IBADA YA JUMAPILI YA KUPAA KWA BWANA KATIKA PAROKIA YA TOLEO LA BWANA JIMBO LA ARUSHA
WATANZANIA WENGI WANAKOSA FURSA ZA KIMAENDELEO KUTOKANA NA KUTOJUA LUGHA
TANZIA DMV NA TANZANIA LETICIA NYERERE HATUNAE TENA.
Waziri Mkuu wa Tanzania ataka majina ya wahusika wa upotevu wa makontena.
Serikali mpya ya Tanzania inaendelea na juhudi zake za kupambana na rushwa nchini humo kwa hatua mbali mbali za viongozi wa juu wa nchi hiyo.
rais John magufuli alikutana na wafanyabiashara wakubwa mjini dar es salaam leo na kuwataka wahakiki ulipaji wao kodi – na endapo una mapungufu basi wailipe serikali kodi ambayo hawajalipa.
Wakat huo huo, Waziri mkuu wa Kassim Majaliwa alifanya ziara nyingine za kushtukiza katika mashirika la bandari na reli mjini dar es salaam na kukagua mfumo wa upokeaji na utoaji mizigo na utozaji wa malipo baada ya kupewa taarifa kwamba kuna makontena 2,431 yaliyotolewa bandarini bila kulipiwa ushuru.
Waziri Mkuu majaliwa alisema kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi wa bandari ya kuanzia Machi hadi Septemba 2014, makontena hayo yalipita bila kulipiwa kodi kupitia bandari kavu nne (ICDs) ambazo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mamlaka ya bandari mpaka sasa imeachisha kazi watumishi 10 tu kutokana na makosa hayo, hali ambayo haikumridhisha waziri mkuu. “Mmeamua kuwasimamisha kazi watu wadogo na kuwaacha wakubwa wanaendelea na kazi. Hatuwezi kuendelea kuikosesha Serikali mapato namna hii,” alisema Waziri Mkuu alisema waziri mkuu.
Kutokana na hivyo Waziri Mkuu Majaliwa amemtaka Kaimu Meneja wa Bandari, Hebel Mhanga ampelekee majina ya watumishi wote waliohusika na ukwepaji kodi huo ifikapo mwisho mwa siku alhamisi. Pia amempa Meneja huyo wiki moja kuhakikisha kuwa mamlaka hiyo inabadilisha mfumo wa utozaji malipo kutoka kwenye maandishi ya karatasi na badala yake kuweka mfumo wa malipo wa kielektroniki (e-payment).
Wakati akikagua idara mbalimbali za mamlaka ya bandari kwenye chumba cha scanner mojawapo, Waziri Mkuu alikuta manifest moja ikisema kontena limejaa nepi za watoto lakini picha ya kwenye kompyuta ya scanner ilionyesha kuwa ndani ya kontena hilo kuna vitu kama vifaa vya umeme.
Katika ziara yake katika shirika la reli Waziri Mkuu Majaliwa alikagua mabehewa na kuzungumza na baadhi ya wafanyakazi waliokuwepo kwenye stesheni hiyo ambako taarifa ya ofisi ya waziri inasema alibaini ufujaji kwenye malipo ya mishahara na makato ya michango ya wafanyakazi.
Akizungumza na Mkurugenzi Mkuu TRL, Elias Mshana, Waziri Mkuu alisema amefika kwenye shirika hilo ili kujifunza utendaji wao kazi lakini anazo taarifa za wao kupewa fedha na Serikali kiasi cha sh. bilioni 13.5/- ili waendeleze miundombinu ya reli lakini hawakufanya hivyo. “Nia ya kuwapa fedha hizo ilikuwa ni kuboresha miradi ili muweze kujiendesha kibiashara lakini nyie mkaamua kujilipa wenyewe,” alisema waziri mkuu.
“Ninazo taarifa kuwa baada ya hapo, mlikopa sh. bilioni 3 kutoka benki ya TIB ili kuendesha miradi ya shirika lakini badala ya kufanya miradi, fedha hizo mkaamua nazo kujilipa mishahara. Sasa sijui mnarudishaje huo mkopo wakati hakuna mradi wowote uliofanyika,” alihoji bila kupata majibu.
Alipoulizwa wafanyakazi wana matatizo gani hapo TRL, Katibu wa TRAWU, Bw. Boaz Nyakeke alisema wanadai malimbikizo ya makato yao kwenye mifuko ya pensheni, malimbikizo ya makato kwenye SACCOS na malimbikizo ya kuanzia Julai – Novemba 2014.
Waziri Mkuu kwa upande wake alimtaka Bw.Mshana asimamie uboreshaji huduma za usafiri wa treni katika Jiji la Dar es Salaam ili hata mabasi ya mwendo kasi yatakapoanza wananchi waweze kuwa na uhuru wa kuchagua aina ya usafiri wautakao.
“Tunataka kujenga yadi kubwa nje ya mji ili watu wenye magari wawe wanayaacha huko na kutumia usafiri wa treni au DART kuja mjini kama njia mojawapo ya kupunguza msongamano wa magari jijini Dar es Salaam,” alisema.
http://www.voaswahili.com
Rais Dkt.John Magufuli akabidhiwa rasmi ofisi na rais mstaafu Kikwete.
Rais Dkt John Pombe Magufuli akipokea kwa furaha hati ya makabadhiano ya Ofisi kutoka kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 12, 2015 |
Magufuli aahidi kuulinda Muungano kwa nguvu zote.
Magufuli ameahidi kuwa akichaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano,atadumisha na
kuulinda Muungano wa Zanzibar na Tanganyika ulioanzishwa na Waasisi wetu
akiwemo Baba wa Taifa Hayati Julius Kambarage Nyerere pamoja na Abeid Amani
Karume.Dkt Magufuli kesho atahutubia kwenye mkutano mkubwa wa kampeni mjini
Unguja.
Mohamed Shein akiwahutubia
wakazi wa Pemba jioni ya leo kwenye kutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja
wa Gombani ya Kale mjini Pemba.Dkt Shein amewataka wakazi wa Kisiwani Pemba
kuilinda amani iliyopo ndani ya kisiwa hicho na kuwa Wananchi wakajitokeze kwa
wingi kupiga kura siku ya Oktoba 25 kwenye uchaguzi mkuu Mwaka huu.
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana Mama Shadia Karume mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Gombani ya Kale kwa ajili ya kuwahutubia wananchi kwenye mkutano wa kampeni.
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza kwa makini Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein kabla ya mkutano wa kampeni kuanza jioni ya leo kisiwani Pemba.
uliofanyika jioni ya leo,kwenye uwanja wa Gombani ya kale kisiwani humo.
wa kiswani Pemba wakishangilia jambo kwenye mkutano wa kampeni
uliofanyika jioni ya leo,ambapo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli pamoja na
Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein
walitumia jukwaa na mkutano huo kuwaomba kura za kutosha ili wakaiongoze
Tanzania katika kipindi cha awamu ya tano.
PICHA NA MICHUZI JR-PEMBA
Normal
0
false
false
false
EN-GB
X-NONE
X-NONE
/* Style Definitions */
table.MsoNormalTable
{mso-style-name:”Table Normal”;
mso-tstyle-rowband-size:0;
mso-tstyle-colband-size:0;
mso-style-noshow:yes;
mso-style-priority:99;
mso-style-parent:””;
mso-padding-alt:0cm 5.4pt 0cm 5.4pt;
mso-para-margin-top:0cm;
mso-para-margin-right:0cm;
mso-para-margin-bottom:10.0pt;
mso-para-margin-left:0cm;
line-height:115%;
mso-pagination:widow-orphan;
font-size:11.0pt;
font-family:”Calibri”,”sans-serif”;
mso-ascii-font-family:Calibri;
mso-ascii-theme-font:minor-latin;
mso-hansi-font-family:Calibri;
mso-hansi-theme-font:minor-latin;
mso-fareast-language:EN-US;}