Waziri Mkuu wa Tanzania ataka majina ya wahusika wa upotevu wa makontena.

b4f123b75846dab06b3f16aec799f0e1
Serikali mpya ya Tanzania inaendelea na juhudi zake za kupambana na rushwa nchini humo kwa hatua mbali mbali za viongozi wa juu wa nchi hiyo.

rais John magufuli alikutana na wafanyabiashara wakubwa mjini dar es salaam leo na kuwataka wahakiki ulipaji wao kodi – na endapo una mapungufu basi wailipe serikali kodi ambayo hawajalipa.

Wakat huo huo, Waziri mkuu wa Kassim Majaliwa alifanya ziara nyingine za kushtukiza katika mashirika la bandari na reli mjini dar es salaam na kukagua mfumo wa upokeaji na utoaji mizigo na utozaji wa malipo baada ya kupewa taarifa kwamba kuna makontena 2,431 yaliyotolewa bandarini bila kulipiwa ushuru.

Waziri Mkuu majaliwa alisema kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi wa bandari ya kuanzia Machi hadi Septemba 2014, makontena hayo yalipita bila kulipiwa kodi kupitia bandari kavu nne (ICDs) ambazo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mamlaka ya bandari mpaka sasa imeachisha kazi watumishi 10 tu kutokana na makosa hayo, hali ambayo haikumridhisha waziri mkuu. “Mmeamua kuwasimamisha kazi watu wadogo na kuwaacha wakubwa wanaendelea na kazi. Hatuwezi kuendelea kuikosesha Serikali mapato namna hii,” alisema Waziri Mkuu alisema waziri mkuu.

Kutokana na hivyo Waziri Mkuu Majaliwa amemtaka Kaimu Meneja wa Bandari, Hebel Mhanga ampelekee majina ya watumishi wote waliohusika na ukwepaji kodi huo ifikapo mwisho mwa siku alhamisi. Pia amempa Meneja huyo wiki moja kuhakikisha kuwa mamlaka hiyo inabadilisha mfumo wa utozaji malipo kutoka kwenye maandishi ya karatasi na badala yake kuweka mfumo wa malipo wa kielektroniki (e-payment).

Wakati akikagua idara mbalimbali za mamlaka ya bandari kwenye chumba cha scanner mojawapo, Waziri Mkuu alikuta manifest moja ikisema kontena limejaa nepi za watoto lakini picha ya kwenye kompyuta ya scanner ilionyesha kuwa ndani ya kontena hilo kuna vitu kama vifaa vya umeme.

Katika ziara yake katika shirika la reli Waziri Mkuu Majaliwa alikagua mabehewa na kuzungumza na baadhi ya wafanyakazi waliokuwepo kwenye stesheni hiyo ambako taarifa ya ofisi ya waziri inasema alibaini ufujaji kwenye malipo ya mishahara na makato ya michango ya wafanyakazi.

Akizungumza na Mkurugenzi Mkuu TRL, Elias Mshana, Waziri Mkuu alisema amefika kwenye shirika hilo ili kujifunza utendaji wao kazi lakini anazo taarifa za wao kupewa fedha na Serikali kiasi cha sh. bilioni 13.5/- ili waendeleze miundombinu ya reli lakini hawakufanya hivyo. “Nia ya kuwapa fedha hizo ilikuwa ni kuboresha miradi ili muweze kujiendesha kibiashara lakini nyie mkaamua kujilipa wenyewe,” alisema waziri mkuu.

“Ninazo taarifa kuwa baada ya hapo, mlikopa sh. bilioni 3 kutoka benki ya TIB ili kuendesha miradi ya shirika lakini badala ya kufanya miradi, fedha hizo mkaamua nazo kujilipa mishahara. Sasa sijui mnarudishaje huo mkopo wakati hakuna mradi wowote uliofanyika,” alihoji bila kupata majibu.

Alipoulizwa wafanyakazi wana matatizo gani hapo TRL, Katibu wa TRAWU, Bw. Boaz Nyakeke alisema wanadai malimbikizo ya makato yao kwenye mifuko ya pensheni, malimbikizo ya makato kwenye SACCOS na malimbikizo ya kuanzia Julai – Novemba 2014.

Waziri Mkuu kwa upande wake alimtaka Bw.Mshana asimamie uboreshaji huduma za usafiri wa treni katika Jiji la Dar es Salaam ili hata mabasi ya mwendo kasi yatakapoanza wananchi waweze kuwa na uhuru wa kuchagua aina ya usafiri wautakao.

“Tunataka kujenga yadi kubwa nje ya mji ili watu wenye magari wawe wanayaacha huko na kutumia usafiri wa treni au DART kuja mjini kama njia mojawapo ya kupunguza msongamano wa magari jijini Dar es Salaam,” alisema.
http://www.voaswahili.com

Rais Dkt.John Magufuli akabidhiwa rasmi ofisi na rais mstaafu Kikwete.

 Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete aliyefika Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi Ofisi ya Rais leo Novemba 12, 2015
  Rais Dkt John Pombe Magufuli akipeana mikono kwa furaha na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete aliyefika Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi Ofisi ya Rais
  Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Obeni Sefue alipofika Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi Ofisi ya Rais
   Rais Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza  Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete aliyefika Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi Ofisi ya Rais. Kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue
  Rais Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza  Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete wakati akiongea kabla ya kukabidhi rasmi Ofisi ya Rais  Ikulu jijini Dar es salaam 
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akipokea kwa furaha hati ya makabadhiano ya Ofisi kutoka kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 12, 2015
Rais Dkt John Pombe Magufuli akipokea kwa furaha hati ya makabadhiano ya Ofisi kutoka kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 12, 2015
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akiiangalia kwa furaha hati ya makabadhiano ya Ofisi aliyoipokea kutoka kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 12, 2015
 Rais Dkt John Pombe Magufuli, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Makiamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na Katibu Mkuu Kiongozi  baada ya hafla ya makabidhiano rasmi ya Ofisi  Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi leo Novemba 12, 2015
Rais Dkt John Pombe Magufuli, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Makiamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan baada ya hafla ya makabidhiano rasmi ya Ofisi  Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi leo Novemba 12, 2015. 
PICHA ZOTE NA ISSA MICHUZI WA IKULU

Uingereza:Mlipuko chanzo ajali ya ndege

151102131111_aviao_russia_reuters_640x360_reuters_nocredit

Mabaki ya ndege ya Urusi ililyoanguka Misri

Uingereza imetoa angalizo kwamba huenda mlipuko ndio uliosababisha ndege ya shirika la ndege la Urusi kuangukia nchini Misri na kuua abiria wote mia mbili na ishirini na wanne waliokuwa kwenye ndege hiyo.

Safari za ndege kati ya nchi za Misri na Uingereza na pwani ya mapumziko ya rasi ya Sharm el-Sheikh zimesitishwa kama tahadhari wakati maofisa kutoka nchini Uingereza wakiendelea kuangalia hali ya usalama katika uwanja wa ndege.

Halikadhalika safari za kutoka na kuingia katika rasi hiyo zimesitishwa na Ireland.

Mamlaka ya safari za anga nchini Urusi hivi karibuni walitoa tahadhari kuwa ni mapema mno kuhisi nini chanzo cha ajali hiyo.

Mabaki ya ndege hiyo na kisanduku cheusi chenye kurekodi mwenendo wa ndege hiyo bado vinafanyiwa uchunguzi.

Mpaka sasa kundi la wanamgambo wa kiislamu, la Islamic State limereudia kukiri kuwa linahusika na ajali hiyo.

-BBC

Romania PM Ponta resigns over Bucharest nightclub fire

Romanian Prime Minister Victor Ponta has resigned, a day after some 20,000 people took to the streets to protest over a nightclub fire that left 32 people dead.

Friday night’s blaze in Bucharest started when a band performing at the club set off fireworks.

Demonstrators called for Mr Ponta to step down, complaining of government corruption and poor safety supervision.

Mr Ponta is already facing trial on corruption charges.

In September, he became the first sitting Romanian prime minister to go on trial over allegations of fraud, tax evasion and money laundering.

He has denied the charges, accusing prosecutors of being “totally unprofessional”.

Mr Ponta said on Wednesday that he and and his government were standing down.

“I hope the government’s resignation will satisfy the people who came out in the streets,” he said on Romanian TV._86496336_86496335 _86495781_029949807-1

-BBC

Magufuli aahidi kuulinda Muungano kwa nguvu zote.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Pemba jioni ya leo kwenye kutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Gombani ya Kale mjini Pemba.

Katika mkutano huo wa Kampeni,Dkt
Magufuli ameahidi kuwa akichaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano,atadumisha na
kuulinda Muungano wa Zanzibar na Tanganyika ulioanzishwa na Waasisi wetu
akiwemo Baba wa Taifa Hayati Julius Kambarage Nyerere pamoja na Abeid Amani
Karume.Dkt Magufuli kesho atahutubia kwenye mkutano mkubwa wa kampeni mjini
Unguja.
Wananchi wa Kisiwani Pemba wakiwa wamekusanyika katika uwanja wa Gombani ya Kale ,wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alipokuwa akijinadi na kuomba kura kwa wananchi hao. 
Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt
Mohamed Shein akiwahutubia
wakazi wa Pemba jioni ya leo kwenye kutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja
wa Gombani ya Kale mjini Pemba.Dkt Shein amewataka wakazi wa Kisiwani Pemba
kuilinda amani iliyopo ndani ya kisiwa hicho na kuwa Wananchi wakajitokeze kwa
wingi kupiga kura siku ya Oktoba 25 kwenye uchaguzi mkuu Mwaka huu.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana Mama Shadia Karume mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Gombani ya Kale kwa ajili ya kuwahutubia wananchi kwenye mkutano wa kampeni.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza kwa makini Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein kabla ya mkutano wa kampeni kuanza jioni ya leo kisiwani Pemba.
Umati wa wakazi wa kisiwani Pemba kwenye mkutano wa kampeni.
Wananchi wa kiswani Pemba wakifuatilia mkutano wa kampeni
uliofanyika jioni ya leo,kwenye uwanja wa Gombani ya kale kisiwani humo.
Wananchi
wa kiswani Pemba wakishangilia jambo kwenye mkutano wa kampeni
uliofanyika jioni ya leo,ambapo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli pamoja na
Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein
walitumia jukwaa na mkutano huo kuwaomba kura za kutosha ili wakaiongoze
Tanzania katika kipindi cha awamu ya tano.

PICHA NA MICHUZI JR-PEMBA

Normal
0

false
false
false

EN-GB
X-NONE
X-NONE

/* Style Definitions */
table.MsoNormalTable
{mso-style-name:”Table Normal”;
mso-tstyle-rowband-size:0;
mso-tstyle-colband-size:0;
mso-style-noshow:yes;
mso-style-priority:99;
mso-style-parent:””;
mso-padding-alt:0cm 5.4pt 0cm 5.4pt;
mso-para-margin-top:0cm;
mso-para-margin-right:0cm;
mso-para-margin-bottom:10.0pt;
mso-para-margin-left:0cm;
line-height:115%;
mso-pagination:widow-orphan;
font-size:11.0pt;
font-family:”Calibri”,”sans-serif”;
mso-ascii-font-family:Calibri;
mso-ascii-theme-font:minor-latin;
mso-hansi-font-family:Calibri;
mso-hansi-theme-font:minor-latin;
mso-fareast-language:EN-US;}

UBA Tanzania celebrated customer service.

Customers and the MD cut the cake to celebrate the Customer Service Week 5-9 October 2015.(All photos by Geofrey Adroph).
Customers toast their glasses in celebration of the Customer Service Week 5–9 October 2015
A cross section of UBA staff with customer of the Bank during the celebration of the Customer Service Week 5 – 9 October 2015.
The Managing Director Mr. Demola Ogunfeyimi addressing UBA staff and Customers at the UBA banking hall at PUGU road during the Customer Service Week celebration.
Mr. Demola Ogunfeyimi the MD of UBA Tanzania hands over gifts to Customers in celebration of the Customer Service Week 5–9 October 2015
Mr. Demola Ogunfeyimi the MD of UBA Tanzania hands over gifts to Customers in celebration of the Customer Service Week 5–9 October 2015
A cross section of UBA staff during the celebration of the Customer Service Week 5 – 9 October 2015.

“I have been banking with UBA since its inception in Tanzania in 2009 and I can say your services are great. I have been receiving first class service, in that manner I have been able to recommend UBA to other businessmen in my circle and I will continue to refer them so they can receive what I am getting from here which excellent customer service” Commented one happy Customers.

UBA Tanzania recognizes this year’s theme as a powerful message for our service teams and entire organization to celebrate during this Customer Service Week. “In celebration of our everyday heroes, we invite all our customers to celebrate with us during this Customer Service Week, October 5-9, 2015” mentioned Queen Odunga the Head of Service Quality.

“Since UBA started in 2009 we had a very small customer base, but now we have managed to open more that 5000 accounts, sold more than 7000 Visa prepaid cards and enrolled a big number of clients on our other E-banking products, i.e. the U-Direct corporate and U-mobile which helps a customer to access financial convenience on their mobile phones or computers wherever they may be, in Tanzania and the rest of the world. This is reason enough for UBA Tanzania to celebrate this Customer service week” Said Madam Flavia Kiyanga the Head of Domestic Operation.

This year’s Customer Service Week theme is “Everyday Heroes” The theme recognizes that every day, frontline customer service professionals are heroes in their customer’s eyes.

Nawashangaa mawaziri wakuu wenzangu waliostaafu wakidai CCM hakuna walichofanya.

 Waziri
Mkuu Mstafu Jaji Joseph Sinde Warioba akihutubia wakazi wa Butiama
ambapo aliwaeleza Magufuli anafaa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.PICHA ZOTE NA MICHUZI JR-MARA
WAZIRI Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba, ameibuka katika
kampeni za mgombea urais wa CCM Dk. John Magufuli na kusema kuwa
anashangazwa na hatua ya mawaziri wakuu wenzake kuhama CCM na kudai
hakuna kilichofanyika katika miaka 54 ya Uhuru.

Pamoja na hali hiyo amesema anajua wazi huenda hata
wanachokifanya hawajui wajibu wao walipokuwa katika madaraka hayo kama
washauri wakuu wa rais.alisema  sasa umefika wakati wa watu
wanaomtumia kama dira Baba wa Taifa katika kampeni zao wajitafakari
zaidi.
“Wengine katika kampeni zao wanatumia maneno ya Mwalimu
kama wamechanganyikiwa. Huwezi kumtumia Mwalimu kama dira halafu unasema
CCM haijafanya kitu, aliijenga Tanzania kwenye misingi na wote
walimfuata wanapita kwenye misingi yake,” alisema Jaji Warioba
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama
cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia mamia ya wananchi
waliojitokeza katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika mjini Bunda
leo.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akipokea kifimbo na Chief Japhet Wanzagi kwa niaba ya Wazee wa Butiama.
 Dkt akionesha fimbo hiyo aliyokabidhiwa na Chief wa Wazanaki,Japhet Wanzagi
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama
cha Mapinduzi Dr. John Pombe Magufuli akiwanadi wagombea ubunge kulia ni
Nimrod Mkono kutoka jimbo la Butiama Vijijini na  Profesa Sospeter
Muhongo ambaye anatoka jimbo la Musoma vijijini.
 Mamia ya Wananchi wakimsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dr. John Pombe
Magufuli.
 Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Nyamuswa ambako ndiko alikozaliwa Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Warioba,wakimsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mgombea Ubunge wa jimbo la Mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe. Stephen Wasira,shoto ni Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba,kwenye mkutano wa kampeni za CCM zilizofanyika mjini Nyamuswa jioni ya leo.
 Wananchi wa Nyamuswa wakimsikiliza Dkt Magufuli.
 Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Nyamuswa ambako ndiko alikozaliwa
Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Warioba,wakimshangilia Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alipokuwa akimwaga sera zake na kuomba ridhaa ya kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano.
  Mgombea
wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akisalimiana na mgombea
ubunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Ndugu Sospeter Muhongo,kushoto ni Mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe. Stephen Wasira wakati wa mapokezi mkoani Mara,pichani kati ni Mtoto wa Baba wa Taifa ambaye pia ni Mbunge wa Afrika Mashariki,Mh Makongoro Nyerere
  Umati wa wakazi wa Butiama wakimsikiliza Mgombea wa Urais wa CCM Dk. John Pombe Magufuli.
 Sehemu ya Wananchi wa Butiama wakishangilia jambo